Misitu Ni Rasilimali

Misitu ni rasilimali

by Consolatha Nicholaus Sileyo

Ninalo langu swali,

nijibuni kwakujali,

itulie yangu hali,

si lazima ni hiyari.


Suali lenyewe  hili,

kwazo  hizi amali,

yupi miliki halali,

Wao au serikali.


nikianza na misitu,

Ipo karibu na watu,

huko ni katazo katu,

hata iingie kiatu.


wamiliki ndio wao,

karibu na miti yao,

walipewa babu zao,

wairithi iwe yao.


Sasa muwaingilie,

mahali mupavamie,

muwambie kwenu nyie

haki wasiwaelewe.


lengo ni kusimamia,

siyo  jingine mwania,

mana walisimamia,

tangu wamewaambia.


Mengi umenikumbusha

Ukweli si kunichosha, 

Ukweli nawapasha, 

Ni ukweli usokisha.


Ile misitu na maji, 

Na mito kama rufiji, 

Ni nyenzo uzaliji, 

O' mali kwa wapigaji.


Udongo pia nishati, 

Ya jua sio ya shoti, 

Umeme ulo simati, 

Ni busara tukaketi.


 langu moja swali, 

Nauliza ukweli, 

Na zitumike akili, 

Kwa jibu li'lokamili.


Misitu ile kukata, 

Tena makazi kupata, 

Siyo sababu ukata, 

Kosa liko wapi?

About

Iā€™m a student, I study archaeology and geography.

Follow Consolatha on Twitter @consolatha26